Pamoja na Dr. Shika kugonga headlines kwa kitendo chake cha kutoa ahadi hewa za kununua nyumba za Lugumi, hafikii hata 1/10 ya kitendo alichowahi kukifanya Msomi Morris Sankuu. Sankuu alizuka miaka ya 1970 kijijini kwetu na kudai kuwa ametokea masomoni Moscow, Urusi. Huyu jamaa alikuwa kila wakati anatembea na matabu makubwa kuliko Dictionary ile ya Kiingereza ya Oxford. Ilikuwa akikutana na mtu mwenye viashiria vya kuwa msomi au mwanafunzi anamwapproach kwa kiingereza, na kuzusha mdahalo wowote naye, lakini kiingereza chake kilikuwa ni kigumu hata cha Prof. Lumumba hakioni ndani. Huyo msomi muda wote alikuwa smart, kuvaa kwake ilikuwa ni mwendo wa suti, tai na viatu aina ya raizoni (enzi hizo raizoni huigusi).
Sasa siku moja alienda kwa uongozi wa kijiji na kuweza kuwashawishi viongozi waitishe mkutano ana mambo muhimu sana anataka kuongea na wananchi. Kutokana na wito wake na approach yake, viongozi wa kijiji chetu walimuunga mkono na kukubaliana kuwa badala ya mkutano uwe wa kijiji, waitwe wananchi kutoka kata nzima. Kwa hiyo ilikuwa ni mshikemshike wa harakati za viongozi wa vijiji kuwaalika wananchi wao. Issue yake ilipewa kiki ikakua zaidi, na kusambaa mpaka eneo la wilaya na mkoa. Nakumbuka majira hayo kulikuwa na mbio za mwenge. Viongozi ngazi za mkoa na wilaya waliazimia kuwa ufanyike mwaliko wa Rais, kwenda kumsikiliza Sankuu kijijini kwetu na sehemu hiyo iwe ndio hitimisho la mbio za mwenge.
Rais (Baba wa Taifa) aliitikia wito kwa mikono miwili. Baada ya mwitikio zilianza shamrashamra za maandalizi ya kumsikiliza Sankuu kijijni kwetu - vikundi vya ngoma, band za wanafunzi, kwata, magawaride nk.
Ilifika siku ya ya Sankuu kusema alichowaitia wananchi mbele ya Rais. Sankuu alikuwa haongei kiswahili ni mwendo wa kiingereza mwanzo mwisho - kitendo hicho kiligrab attention za watu na kusababisha Rais badala ya kumsikiliza akageuka kuwa mkalimani! Rais alibabaika kukalimani, hadi akawa akisubiri Sankuu aongee na kutafsiri kijumlajumla.
Msomi Sankuu aliwahutubia wananchi kupitia ukalimani wa Baba wa Taifa. Alijitambulisha kama msomi wa sayansi ya mambo ya anga kutoka Urusi. Huko amehitimu masomo ya juu zaidi na kuajiriwa kufanya kazi katika viwanda vya kutengeneza ndege na rocket. Kwamba ameongea na serikali ya Urusi na wamekubali kumpa ndege mbili kwa ajili ya Tanzania na meli 2 ambazo zitaanza safari ya kuja nchini iwapo Rais angeridhia. Wananchi pamoja na Rais walisisimkwa sana na ahadi za Sankuu.
Lakini kuna jambo moja alimaliza nalo. Akasema pamoja na kwamba mimi naleta ndege na meli ambazo zitakuwa mali ya Taifa, nimeahidiwa mabasi matatu kwa ajili ya kijiji. Lakini sitakubali yaje bila kuwa na barabara zinazoeleweka. Rais aliahidi ndani ya muda sifuri kwenda kushughulikia bajeti ya kujenga barabara kijijini kwetu mpaka makao makuu ya mkoa ambayo ilikuwa ni mjini.
Hadi hivi sasa ninapomaliza kuandika, barabara za kijijini kwetu ni lami ambayo ipo tangu miaka ya 1970.
Sankuu baada ya hotuba yake na ziara ya Rais, aliahidi kuwa kuanzia kesho yake ataanza mchakato wa kufuatilia Meli, ndege na Mabasi, lakini mchakato huo angeufanya akiwa Moscow, hivyo hakuonekana tena mpaka hivi sasa.
Naamini Nyerere ilikuwa akikumbuka kitendo cha Sankuu alicheka mwenyewe mpaka hadi kupaliwa.
Sankuu ndio mtu pekee tu ambaye kila nikimtafakari huwa simumalizi.
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 10 hours ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 328 Views 37779
- by Eli 10 hours ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 705 Views 303512
- by Eli 4 days ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 663 Views 238509
- by Eli 6 days ago PySpark for Large Data Processing View the latest post Replies 1 Views 7934
- by Eli 1 week ago President Museveni's Speech During International Development Association (IDA) Summit View the latest post Replies 1 Views 325
- by Eli 1 week ago From Simple Linear Regression Analysis to Covariance & Correlation to Independent Determinant, and R-Squared View the latest post Replies 11 Views 24934
- by Eli 2 weeks ago Collection of Greatest Christian Hymns of all Times View the latest post Replies 34 Views 70485
- by Eli 2 weeks ago Pondering Big Cosmology Questions Through Lectures and Dialogues View the latest post Replies 34 Views 58502
- by Eli 2 weeks ago Programmatically Manipulate Files: Renaming, Reading, Writing, Deleting, and Moving Files Between Folders View the latest post Replies 7 Views 18594
- by Eli 3 weeks ago Iran Launches Retaliatory Attack Against Israel, and Israel Retaliates by Attacking Iranian Isfahan Millitary Base View the latest post Replies 28 Views 20911
-
Dr. Shika Ametisha Lakini Hafikii Hata 1/10 ya Kitendo Alichowahi Kukifanya Morris Sankuu
- Eli
- Senior Expert Member
- Reactions: 183
- Posts: 5387
- Joined: 9 years ago
- Location: Tanzania
- Has thanked: 75 times
- Been thanked: 88 times
- Contact:
Dr. Shika sio wa mchezo, viewtopic.php?f=196&t=5598&sid=e7ca9737 ... 2991bfa3c0
@Simulink
@RealityKing Story ya Shika umeiachia njiani, iendeleze bado kuna mengi, anazidi kutoa episodes.
Critical Thinkers, sasa hivi unaweza kukopi na kupaste au kuandika tu web address fulani, then info kutoka website husika zitakuwa pulled na dislayed magically: Kwa mfano, jaribu kuandika websites za Google, Facebook, Twitter:
www.google.com
www.facebook.com
www.twitter.com
Inapendeza sasa.
@Simulink
@RealityKing Story ya Shika umeiachia njiani, iendeleze bado kuna mengi, anazidi kutoa episodes.
Critical Thinkers, sasa hivi unaweza kukopi na kupaste au kuandika tu web address fulani, then info kutoka website husika zitakuwa pulled na dislayed magically: Kwa mfano, jaribu kuandika websites za Google, Facebook, Twitter:
www.google.com
www.facebook.com
www.twitter.com
Inapendeza sasa.
0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 1 guest