Wakati Serikali ikihaha kuandaa mwongozo kwa vyuo na shule binafsi za msingi na sekondari ili kudhibiti viwango vya ada, hali ni tofauti kwenye shule za kimataifa ambazo zinaonekana kama zinachuana kwa kuwa na ada kubwa.
Wakati ada ya juu kwa shule zinazotumia Kiingereza kuanzia elimu ya msingi ni kati ya Sh 2 milioni na Sh 3 milioni, ada ya shule za kimataifa zilizopo nchini inafikia hadi Sh 60 milioni kwa mwaka, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mwananchi kwenye shule mbalimbali za jijini Dar es Salaam na baadhi ya mikoa.
Uchunguzi huo unaonyesha kuwa mwanafunzi wa chekechea hutakiwa kulipa hadi Sh 35 milioni kwa mwaka na fedha hizo hulipwa kwa kutumia dola za Kimarekani.
Baadhi ya shule zinapokea wanafunzi wenye asili ya Asia, nyingine hupokea wanafunzi kutoka nchi tofauti bila ya kubagua na ni dhahiri kuwa hata wazazi wa watoto ni wale wa kipato kikubwa.
Shule nyingi zinatumia Kiingereza katika kufundisha masomo yote darasani kwa mitaala ya kimataifa na walimu wa kigeni ambao wanalipwa mishahara kwa viwango vya kimataifa.
Wanafunzi wanaosoma katika shule hizo wanaishi mazingira tofauti na wanaosoma katika shule za kawaida. Mwananchi lilishuhudia baadhi ya wanafunzi wa kike wakiwa wamevaa kaptula, bukta na sketi zinazoacha wazi mapaja, kufuga rasta huku wavulana wakiwa huru kufuga nywele, na kuvaa hereni bila kubanwa na sheria.
Ada na Michango ya Shule
Kwa kuzingatia nyaraka za kujiunga na shule ya International School of Tanganyika (IST) (Shule nyingine inayofanana na IST ni International School of Moshi) iliyoko Masaki, ada ya mwanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa pili wa chekechea ni Sh 35.9 milioni; darasa la tatu hadi la tano ada ni Sh 39.8 milioni na kwa wale wanaoingia darasa la sita, la saba na la nane ni Sh 46. 3 milioni huku darasa la tisa na la kumi ada ni Sh 49.2 milioni.
Mchanganuo wa ada kwa mwanafunzi anayeingia darasa la 11 na 12 ni Sh 59.4 milioni. Mbali ya ada hiyo, mwanafunzi hutakiwa pia kulipiwa gharama za ujenzi, ada ya dharura, fomu ya kujiunga shuleni pamoja na michango mingine ambavyo jumla ni Sh 19.8 milioni.
Shule nyingine ambayo tozo zake - ada na michango mingine – imefuata mkondo huo ni Braeburn iliyoko barabara ya Bagamoyo, Africana. Ada ya mwanafunzi wa chekechea ni Sh 12.7 milioni kwa mwaka.
Mwaka wa kwanza na wa pili ambao ni sawa na darasa la kwanza na la pili hulipa Sh 19.3 milioni. Darasa la tatu hadi la sita Sh 21.1 milioni na darasa la saba hadi la tisa (sekondari) ni Sh 25.4 milioni. Mwanafunzi anayejiunga na shule ya msingi ya Readers Rabbit iliyoko Masaki hutakiwa kulipa kiasi cha Sh 24.1 milioni kwa mwaka.
Soma zaidi hapa: Shule Dar yatoza Sh 60 milioni
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 8 hours ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 326 Views 31805
- by Eli 1 day ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 662 Views 232781
- by Eli 1 day ago PySpark for Large Data Processing View the latest post Replies 1 Views 4373
- by Eli 3 days ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 700 Views 297454
- by Eli 6 days ago President Museveni's Speech During International Development Association (IDA) Summit View the latest post Replies 1 Views 252
- by Eli 6 days ago From Simple Linear Regression Analysis to Covariance & Correlation to Independent Determinant, and R-Squared View the latest post Replies 11 Views 24716
- by Eli 1 week ago Collection of Greatest Christian Hymns of all Times View the latest post Replies 34 Views 65134
- by Eli 1 week ago Pondering Big Cosmology Questions Through Lectures and Dialogues View the latest post Replies 34 Views 57942
- by Eli 1 week ago Programmatically Manipulate Files: Renaming, Reading, Writing, Deleting, and Moving Files Between Folders View the latest post Replies 7 Views 13666
- by Eli 2 weeks ago Iran Launches Retaliatory Attack Against Israel, and Israel Retaliates by Attacking Iranian Isfahan Millitary Base View the latest post Replies 28 Views 14978
-
Baadhi ya Shule Tanzania Hutoza Ada na Michango kati ya Milioni 60 na Milioni 100
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 0 guests