Biashara ya kilimo na ufugaji nchini Tanzania huenda miaka michache ijayo ikawa na tija katika kuajiri na kuchangia pato la Taifa kuliko ambavyo imekuwa kwa miaka mingi. Sekta za kilimo na ufugaji nchini Tanzania hazijapewa kipaumbele na serikali kwa kiwango kinachostahili hasa ukizingatia ni sekta zinazoajiri watanzania zaidi ya asilimia 80.
Hata hivyo mambo huenda yakabadilika miaka kadhaa ijayo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na watu maarufu kuanza kuonyesha njia kwa kufanya kilimo cha kisasa. Mfano wa watu hao ni aliyekuwa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye hivi sasa ni mkulima na mfugaji wa ng'ombe.
Mwingine ni Salumu Sumry, aliyekuwa mmiliki wa mabasi ya Sumry ambaye ameachana na biashara ya usafiri wa mabasi na kujiingiza katika biashara ya kilimo, hasa cha mahindi. Salumu aliachana na biashara ya mabasi, wakati huo akiwa anamiliki mabasi 81.
Vilevile kuna habari za uhakika kuwa Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne, ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda, naye ni mkulima na mfugaji hivi sasa.
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 1 day ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 689 Views 277385
- by Eli 3 days ago Iran Launches Retaliatory Attack Against Israel, and Israel Retaliates by Attacking Iranian Isfahan Millitary Base View the latest post Replies 28 Views 941
- by Eli 5 days ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 319 Views 12328
- by Eli 1 week ago Python Packages for Scientific Computing View the latest post Replies 8 Views 6041
- by Eli 1 week ago Dunia Yetu: Building Tanzania's Digital Future Together View the latest post Replies 5 Views 1888
- by Eli 1 week ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 646 Views 213801
- by Eli 1 week ago Programmatically Move Files from One Folder to Another View the latest post Replies 6 Views 1451
- by Eli 2 weeks ago Collection of Greatest Christian Hymns of all Times View the latest post Replies 33 Views 46928
- by Eli 2 weeks ago What is Retrieval-Augmented Generation (RAG)? View the latest post Replies 2 Views 369
- by Eli 2 weeks ago Chat With ChatGPT - An Interactive Conversational AI View the latest post Replies 22 Views 27664
-
Kilimo na Ufugaji, Jakaya Kikwete, Salumu Sumry na Mizengo Pinda Waonyesha Njia
-
- Expert Member
- Reactions: 23
- Posts: 55
- Joined: 7 years ago
- Has thanked: 14 times
- Been thanked: 28 times
- Contact:
Ni jambo jema sana hili, ninachoona ni kuwa watu wenye kipato cha wastani ni changamoto kwao kufanya kilimo kama hiki. Mtaji na nia inahitajika. Halafu kile kilimo cha kupiga simu shamba huku ukiwa mjini ni patapotea pia.
0
- Eli
- Senior Expert Member
- Reactions: 183
- Posts: 5334
- Joined: 9 years ago
- Location: Tanzania
- Has thanked: 75 times
- Been thanked: 88 times
- Contact:
@Simulink
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 3 guests