Biashara ya kilimo na ufugaji nchini Tanzania huenda miaka michache ijayo ikawa na tija katika kuajiri na kuchangia pato la Taifa kuliko ambavyo imekuwa kwa miaka mingi. Sekta za kilimo na ufugaji nchini Tanzania hazijapewa kipaumbele na serikali kwa kiwango kinachostahili hasa ukizingatia ni sekta zinazoajiri watanzania zaidi ya asilimia 80.
Hata hivyo mambo huenda yakabadilika miaka kadhaa ijayo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na watu maarufu kuanza kuonyesha njia kwa kufanya kilimo cha kisasa. Mfano wa watu hao ni aliyekuwa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye hivi sasa ni mkulima na mfugaji wa ng'ombe.
Mwingine ni Salumu Sumry, aliyekuwa mmiliki wa mabasi ya Sumry ambaye ameachana na biashara ya usafiri wa mabasi na kujiingiza katika biashara ya kilimo, hasa cha mahindi. Salumu aliachana na biashara ya mabasi, wakati huo akiwa anamiliki mabasi 81.
Vilevile kuna habari za uhakika kuwa Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne, ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda, naye ni mkulima na mfugaji hivi sasa.
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 30 minutes ago Inaugural Lecture by Prof. Mukandala: Dola, Soko na Kushindwa kwa Taasisi View the latest post Replies 1 Views 22
- by Eli 1 day ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 332 Views 40676
- by Eli 1 day ago Iran's President Ebrahim Raisi Aged 63 Dies in a Helicopter Crash View the latest post Replies 3 Views 65
- by Eli 1 day ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 717 Views 307458
- by Eli 3 days ago PySpark for Large Data Processing View the latest post Replies 2 Views 8173
- by Eli 3 days ago Online Bible View the latest post Replies 3 Views 23331
- by Eli 4 days ago Generating SSH Key and Adding it to the ssh-agent for Authentication on GitHub View the latest post Replies 1 Views 495
- by Eli 1 week ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 663 Views 241290
- by Eli 2 weeks ago President Museveni's Speech During International Development Association (IDA) Summit View the latest post Replies 1 Views 509
- by Eli 2 weeks ago From Simple Linear Regression Analysis to Covariance & Correlation to Independent Determinant, and R-Squared View the latest post Replies 11 Views 25146
-
Kilimo na Ufugaji, Jakaya Kikwete, Salumu Sumry na Mizengo Pinda Waonyesha Njia
-
- Expert Member
- Reactions: 23
- Posts: 55
- Joined: 7 years ago
- Has thanked: 14 times
- Been thanked: 28 times
- Contact:
Ni jambo jema sana hili, ninachoona ni kuwa watu wenye kipato cha wastani ni changamoto kwao kufanya kilimo kama hiki. Mtaji na nia inahitajika. Halafu kile kilimo cha kupiga simu shamba huku ukiwa mjini ni patapotea pia.
0
- Eli
- Senior Expert Member
- Reactions: 183
- Posts: 5411
- Joined: 9 years ago
- Location: Tanzania
- Has thanked: 75 times
- Been thanked: 88 times
- Contact:
@Simulink
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 0 guests