Habari wadau,
Nina wazo kuwa watu wote ambao wanapenda kujifunza namna ya kudevelop applications mbalimbali - desktop, mobile, cloud au vyovyote vile na wale ambao wamebobea katika kudevelop software mbalimbali wafungue community public repositories GitHub kwa ajili ya kujifunza na kushirikiana namna ya kudevelop applications. Hii itawezesha developers waliobobea kuwa mentors kwa wengine na wale ambao wanajifunza hata kama kuanzia hatua za mwanzoni kabisa kufundishwa na kujifunza.
Haihitaji kuanza kudevelop app au system ambayo ni complicated sana, bali kuanza tu kujifunza basics na kuendelea hatua kwa hatua.
Kuanza kwanza kwa kufahamu matumizi ya Git na GitHub itakuwa ndio msingi wenyewe.
Nina amini kuna watu wengi humu wenye nia ya kufundisha, pia wapo wengi wenye nia ya kujifunza.
Hii ni njia nzuri ya kutengeneza online community ya developers/software engineers hasa wa Kitanzania.
Usije na wazo kwamba nilishajaribu ikashindikana na malalamiko mengine ya namna hiyo, njoo na wazo la namna gani hii online community ya developers ninayoifikiria mimi inaweza kuwa successful na sustainable.
Kuwa na online community ya developers sio tu ni njia ya kujifunza na kufundishana, bali itatoa ajira kwa watu kwa sababu watu wataona uwezo wako, na pindi mtu au kampuni itakapohitaji app au maarifa yako, basi itakuwa ni nafasi nzuri ya wewe kupata tender/ajira.
Baadaye tutakuja kuwa na events kama BootCamps, coding competitions - na kutoa zawadi mbalimbali kumotivate developers na wale wanaojifunza, get together, na ikiwezekana digital lab yetu - yaani sehemu ambapo tutaweza kuonana physically kwa ajili ya mihadhara, developments, hands-on training/mentorship, kusolve challenges mbalimbali na kadhalika.
Tuache kulalamika, kama kweli tupo serious, "let's take an adavantage of an upcoming industrial sector in Tanzania" - kumbuka kama nchi itaendea kuwa ya viwanda, kutakuwa na massive need ya applications, software na systems mbalimbali kwa ajili ya kuendesha viwanda - kuanzia kwenye operations, monitoring, control, management, production, service provisions, etc.,.
Nasubiri michango na maoni yenu.
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 5 hours ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 323 Views 23412
- by Eli 1 day ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 697 Views 288470
- by Eli 2 days ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 655 Views 224296
- by Eli 3 days ago Collection of Greatest Christian Hymns of all Times View the latest post Replies 34 Views 57282
- by Eli 3 days ago Pondering Big Cosmology Questions Through Lectures and Dialogues View the latest post Replies 34 Views 57574
- by Eli 4 days ago Programmatically Manipulate Files: Renaming, Reading, Writing, Deleting, and Moving Files Between Folders View the latest post Replies 7 Views 6335
- by Eli 1 week ago Iran Launches Retaliatory Attack Against Israel, and Israel Retaliates by Attacking Iranian Isfahan Millitary Base View the latest post Replies 28 Views 5895
- by Eli 2 weeks ago Python Packages for Scientific Computing View the latest post Replies 8 Views 12562
- by Eli 2 weeks ago Dunia Yetu: Building Tanzania's Digital Future Together View the latest post Replies 5 Views 3383
- by Eli 3 weeks ago What is Retrieval-Augmented Generation (RAG)? View the latest post Replies 2 Views 5104
-
Tanzania software engineers/developers GitHub Community
- Eli
- Senior Expert Member
- Reactions: 183
- Posts: 5362
- Joined: 9 years ago
- Location: Tanzania
- Has thanked: 75 times
- Been thanked: 88 times
- Contact:
Here is a Github account we have created for software developers, programmers, coders, e.tc.,
https://github.com/TSSFL
https://github.com/TSSFL
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 0 guests