• Active Topics 

Kilimo na Ufugaji, Jakaya Kikwete, Salumu Sumry na Mizengo Pinda Waonyesha Njia

This sub-platform is all about risk taking functions. Help others to learn how to develop unique business ideas, acquire resources and dare for success!
Post Reply
RealityKing
Senior Expert Member
Reactions: 26
Posts: 163
Joined: 7 years ago
Has thanked: 10 times
Been thanked: 14 times

#1

Biashara ya kilimo na ufugaji nchini Tanzania huenda miaka michache ijayo ikawa na tija katika kuajiri na kuchangia pato la Taifa kuliko ambavyo imekuwa kwa miaka mingi. Sekta za kilimo na ufugaji nchini Tanzania hazijapewa kipaumbele na serikali kwa kiwango kinachostahili hasa ukizingatia ni sekta zinazoajiri watanzania zaidi ya asilimia 80.

Hata hivyo mambo huenda yakabadilika miaka kadhaa ijayo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na watu maarufu kuanza kuonyesha njia kwa kufanya kilimo cha kisasa. Mfano wa watu hao ni aliyekuwa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye hivi sasa ni mkulima na mfugaji wa ng'ombe.



Mwingine ni Salumu Sumry, aliyekuwa mmiliki wa mabasi ya Sumry ambaye ameachana na biashara ya usafiri wa mabasi na kujiingiza katika biashara ya kilimo, hasa cha mahindi. Salumu aliachana na biashara ya mabasi, wakati huo akiwa anamiliki mabasi 81.



Vilevile kuna habari za uhakika kuwa Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne, ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda, naye ni mkulima na mfugaji hivi sasa.

1
1 Image
Joseph Bundala
Expert Member
Reactions: 23
Posts: 55
Joined: 7 years ago
Has thanked: 14 times
Been thanked: 28 times
Contact:

#2

Ni jambo jema sana hili, ninachoona ni kuwa watu wenye kipato cha wastani ni changamoto kwao kufanya kilimo kama hiki. Mtaji na nia inahitajika. Halafu kile kilimo cha kupiga simu shamba huku ukiwa mjini ni patapotea pia.
0
User avatar
Eli
Senior Expert Member
Reactions: 183
Posts: 5211
Joined: 9 years ago
Location: Tanzania
Has thanked: 75 times
Been thanked: 88 times
Contact:

#3

@Simulink

Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
User avatar
Eli
Senior Expert Member
Reactions: 183
Posts: 5211
Joined: 9 years ago
Location: Tanzania
Has thanked: 75 times
Been thanked: 88 times
Contact:

#4

0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
Post Reply

Return to “Entrepreneurship, Business, Economy”

  • Information
  • Who is online

    Users browsing this forum: No registered users and 0 guests