Biashara ya kilimo na ufugaji nchini Tanzania huenda miaka michache ijayo ikawa na tija katika kuajiri na kuchangia pato la Taifa kuliko ambavyo imekuwa kwa miaka mingi. Sekta za kilimo na ufugaji nchini Tanzania hazijapewa kipaumbele na serikali kwa kiwango kinachostahili hasa ukizingatia ni sekta zinazoajiri watanzania zaidi ya asilimia 80.
Hata hivyo mambo huenda yakabadilika miaka kadhaa ijayo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na watu maarufu kuanza kuonyesha njia kwa kufanya kilimo cha kisasa. Mfano wa watu hao ni aliyekuwa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye hivi sasa ni mkulima na mfugaji wa ng'ombe.
Mwingine ni Salumu Sumry, aliyekuwa mmiliki wa mabasi ya Sumry ambaye ameachana na biashara ya usafiri wa mabasi na kujiingiza katika biashara ya kilimo, hasa cha mahindi. Salumu aliachana na biashara ya mabasi, wakati huo akiwa anamiliki mabasi 81.
Vilevile kuna habari za uhakika kuwa Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne, ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda, naye ni mkulima na mfugaji hivi sasa.
-
- Active Topics
-
-
- by Eli 8 hours ago Re: What is in Your Mind? View the latest post Replies 732 Views 331550
- by Eli 18 hours ago Russia Invades Ukraine View the latest post Replies 674 Views 265138
- by Eli 20 hours ago All in One: YouTube, TED, X, Facebook and Instagram Reels, Videos, Images and Text Posts View the latest post Replies 334 Views 54918
- by Eli 4 days ago Shared Images View the latest post Replies 6 Views 1669
- by Eli 6 days ago Dr Wahome: How World Health Organization (WHO) is Doing Bad Things View the latest post Replies 1 Views 242
- by Eli 1 week ago Introduction to Abstract Algebra View the latest post Replies 4 Views 11183
- by Eli 1 week ago Generating SSH Key and Adding it to the ssh-agent for Authentication on GitHub View the latest post Replies 2 Views 1332
- by Eli 1 week ago How AI Could Empower any Business View the latest post Replies 1 Views 442
- by Eli 1 week ago Pondering Big Cosmology Questions Through Lectures and Dialogues View the latest post Replies 35 Views 62637
- by Eli 1 week ago The U.S - China Rivalry, Taiwan and Hong Kong View the latest post Replies 1 Views 576
-
Kilimo na Ufugaji, Jakaya Kikwete, Salumu Sumry na Mizengo Pinda Waonyesha Njia
-
- Expert Member
- Reactions: 23
- Posts: 55
- Joined: 7 years ago
- Has thanked: 14 times
- Been thanked: 28 times
- Contact:
Ni jambo jema sana hili, ninachoona ni kuwa watu wenye kipato cha wastani ni changamoto kwao kufanya kilimo kama hiki. Mtaji na nia inahitajika. Halafu kile kilimo cha kupiga simu shamba huku ukiwa mjini ni patapotea pia.
0
- Eli
- Senior Expert Member
- Reactions: 185
- Posts: 5461
- Joined: 9 years ago
- Location: Tanzania
- Has thanked: 75 times
- Been thanked: 88 times
- Contact:
@Simulink
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
Kilimo unatakiwa ujipeleke mwenyewe na usimamie kwelikweli. Bado naamini kuwa serikali yetu inatakiwa kutoa kipaumbele cha kipekee katika sekta ya kilimo kwa sababu ndiyo inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania.
0
TSSFL -- A Creative Journey Towards Infinite Possibilities!
-
- Information
-
Who is online
Users browsing this forum: No registered users and 0 guests